Mwenyekiti wa bunge Mussa Azzan Zungu amewataka wabunge kujielekeza katika mjadala wa bajeti uliopo bungeni kwa sasa badala ya kutumia nafasi hiyo kuwashambulia viongozi wastaafu waliotumia nguvu na uwezo wao kuitumikia nchi hii.

In Kitaifa

Mwenyekiti wa bunge Mussa Azzan Zungu amewataka wabunge kujielekeza katika mjadala wa bajeti uliopo bungeni kwa sasa badala ya kutumia nafasi hiyo kuwashambulia viongozi wastaafu waliotumia nguvu na uwezo wao kuitumikia nchi hii.

Agizo la ZUNGU limefuatia baada ya baadhi ya wabunge kuanzia jana kuwataja marais wastaafu na kuwahusisha na masuala mbalimbali yanayoendelea katika sekta ya madini nchini huku wakitaka wachukuliwe hatua.

Akitoa angalizo hilo jana  bungeni mjini Dodoma ZUNGU amesema Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, inatoa kinga kwa rais aliye madarakani na hata rais mstaafu kushtakiwa au kufungua mahakamani shauri yoyote ya jinai dhidi yake.

Mwenyekiti huyo amesema mtu yoyote ambaye hatahusika katika sakata hilo, sio lazima kumtaja ndani ya bunge kwa kuwa atashughulikiwa na vyombo husika.

Agizo la ZUNGU limefuatia mwongozo ulioombwa na waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu sera,bunge,kazi,vijana,ajira na watu wenye ulemavu JENISTA MHAGAMA ambaye ametaka kujua kama ni sahihi kwa wabunge kuendelea kuwatuhumu marais wastaafu kwa kuwataka washtakiwe kuhusiana na suala la mchanga.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu