Mwigulu Nchemba amezitaka jamii za kifugaji kuwapeleka watoto shule.

In Kitaifa

Waziri wa Mambo ya ndani, Mwigulu Nchemba amewataka wananchi wa jimboni la Iramba Magharibi, wa jamii ya kifugaji kuachana na  tamaduni za kutowapeleka watoto shule na kuwatumikisha kufuga mifugo yao.

Akizungumza wakati ziara yake jimboni Mwigulu amesema kuwa Urithi ulio mkubwa zaidi kwa mtoto ni Elimu,ambayo itamasaidia mtoto kwa maisha yake ya baadae.

Nchemba amezitaka jamii hizo kuachana na tamaduni ambazo zimepitwa na wakati kwani hali ya maisha imebadilika tofauti na miaka iliyopita.

Aidha amewataka kufuga kisasa kwa tija zaidi tofauti na hapo awali kutokana na mabadiliko ya tabia nchi yanasababisha ukame hivyo amewaasa kuwekeza katika elimu kwa kuwapeleka watoto shule ili waje kuwa msaada kwa baadaye.

Hata hivyo, katika ziara yake hiyo ya jimboni kwake, Nchemba ametembelea ujenzi wa hosteli katika kila shule ya Sekondari katika Kata 20 na kujionea maendeleo ya ujenzi huo ambao unaendelea kwa kasi kubwa

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu