Mwigulu Nchemba amezitaka jamii za kifugaji kuwapeleka watoto shule.

In Kitaifa

Waziri wa Mambo ya ndani, Mwigulu Nchemba amewataka wananchi wa jimboni la Iramba Magharibi, wa jamii ya kifugaji kuachana na  tamaduni za kutowapeleka watoto shule na kuwatumikisha kufuga mifugo yao.

Akizungumza wakati ziara yake jimboni Mwigulu amesema kuwa Urithi ulio mkubwa zaidi kwa mtoto ni Elimu,ambayo itamasaidia mtoto kwa maisha yake ya baadae.

Nchemba amezitaka jamii hizo kuachana na tamaduni ambazo zimepitwa na wakati kwani hali ya maisha imebadilika tofauti na miaka iliyopita.

Aidha amewataka kufuga kisasa kwa tija zaidi tofauti na hapo awali kutokana na mabadiliko ya tabia nchi yanasababisha ukame hivyo amewaasa kuwekeza katika elimu kwa kuwapeleka watoto shule ili waje kuwa msaada kwa baadaye.

Hata hivyo, katika ziara yake hiyo ya jimboni kwake, Nchemba ametembelea ujenzi wa hosteli katika kila shule ya Sekondari katika Kata 20 na kujionea maendeleo ya ujenzi huo ambao unaendelea kwa kasi kubwa

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu