Mwigulu Nchemba asema Wizara yake inashughulikia suala la kutekwa kwa ROMA

In Kitaifa

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba amesema wizara yake inafuatilia kwa karibu kubaini watekaji na watu wanaokamata na kuchukuliwa watu wengine nchini.

Kauli hiyo aliitoa mjini Dodoma wakati wa mahojiano na vyombo vya habari nje ya Ukumbi wa Bunge baada ya wabunge kuitaka serikali itoe tamko kutokana vitendo ya utekaji na kuchukuliwa watu kuendelea kujitokeza nchini.

“Tayari wizara yangu inashughulikia suala hilo la kutekwa msanii Roma Mkatoliki na kuchunguza ili kuona ni nani anahusika katika utekaji huo, kwani anaweza kuwa asiwe askari na mtu mwingine akatumia mavazi ya askari kufanya utekaji huo,” alieleza Mwigulu.

Mwigulu alisema kama serikali kupitia wizara yake inatakiwa kufanya mambo kwa uhakika pamoja na kuchunguza ndipo itoe taarifa kuhusu jambo lolote.

Alisema tayari wizara yake imechukua hatua za kuchunguza jambo hilo la msaniii Roma.

Ndani ya Bunge wakati wakichangia Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, wabunge waliuliza kwanini serikali inanyamaza kimya kutoa tamko wakati wimbi la kutekwa watu na kukamatwa na kupotea bila kueleweka wapo wapi linaendelea kutokea nchini.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu