Mzingira nchini Somalia yaimarika na kufaulu kufanya mambo yake.

In Kimataifa

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, ameambia kikao cha kimataifa kinachojadiliana hatma ya Somalia kuwa mazingira nchini Somalia hivi sasa yameimarika na kwamba taifa hilo linaweza kufaulu katika yale linalotaka kufanya.

Amesema nchi hiyo kwa sasa ina serikali ambayo inaweza kuaminika na mipango yenye maana.

Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema Jumuia ya Kimataifa ina nafasi kubwa kuisaidia Somalia.

Hata hivyo Rais wa Somalia Mohamed Abdullahi Mohamed Farmajo ameonya kuwa mapambano dhidi ya wapiganaji wa Al Shabaab yanaweza kuendelea kwa miongo kadhaa iwapo vikwazo vya silaha havitaondolewa.

Mkutano huo wa siku moja ulizungumzia pia tatizo linaloikabili Somalia la athari za ukame ambazo zinageuka kuwa baa la njaa.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Maagizo ya wizara kuhusu mfuko wa maendeleo ya kilimo.

Naibu Waziri Wa Kilimo Anthony Mavunde, amesema serikaliimeanza kutekeleza uanzishwaji wa mfuko wa maendeleo yakilimo utakaosaidia kukabiliana na changamoto

Read More...

TANZIA: WAZIRI MSTAAFU WA KILIMO AFARIKI DUNIA

Aliyewahi kuwa mbunge wa jimbo la Musoma Vijijini na Waziri wa Kilimo na Mifugo Mhe. Herman Kirigini Amefariki Dunia. Akithibitisha

Read More...

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Professor Makame Mbarawaameliomba Bunge kumuidhinishia kiasi cha Sh Trilioni 3.6ikiwa ni makadirio ya mapato

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu