Naibu Meya wa Jiji la Arusha afunga mafunzo ya kisheria kwa wanawake wajane na watoto yatima.

In Kitaifa

Naibu Meya wa Jiji la Arusha Mhe.Viola Likindikoki leo Oktoba 24 amefunga mafunzo ya kisheria katika kata ya Moivaro kwa kuwatunuku vyeti wanawake wajane wanaotoka ndani na nje ya kata ya Moivaro pamoja na watoto yatima wanaotoka katika kituo cha Tumaini vocetion training center.

Mafunzo hayo ya kisheria yaliandaliwa na  Bi.Judy Owens na kufanyika katika kanisa la International evangelist Church,Pia Bi.Judy ndiye alikua Mkufunzi katika mafunzo hayo.Hata hivyo Mawakili walialikwa ili kutoa somo la kisheria katika mafunzo hayo,miongoni mwa mawakili walioalikwa ni Bi.Winniefrida Manyanga na Baraka Joel.

Mafunzo hayo ya kisheria yalifunguliwa miezi mitatu iliyopita na Diwani wa kata hiyo Mhe.Rick Moiro.

Wanawake hao wajane waliopokea Mafunzo hayo ya kisheria wametakiwa kwenda kuwafundisha wanawake wengine wajane wanaokaa ndani na nje ya kata hiyo waliokosa fursa ya kupata mafunzo hayo.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Serikali kuunga mkono juhudi za Taasisi mbali mbali.

Rais wa Zanzibar Dkt Hussein Mwinyi, amesema serikaliitaendelea kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Taasisi yaZanzibar Maisha Bora Foundation,pamoja na

Read More...

DKT. KIRUSWA AZINDUA MFUMO WA USHIRIKISHWAJI WA WATANZANIA KATIKA SEKTA YA MADINI

Watanzania waendelea kunufaika Sekta ya Madini, ajira 15,341 zamwagwa, manunuzi ya ndani ya nchi yafikia Dola za Marekani bilioni

Read More...

MAFURIKO YAUWA 190 MALAWI

Takriban watu 190 sasa wamethibitishwa kufariki nchini Malawi baada ya Dhoruba ya Mafuriko ya Tropiki Freddy kulikumba eneo

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu