Naibu waziri wa nishati na madini aagiza wateja mkoani Mwanza wafungie umeme kabla ya julai 25.

In Kitaifa

Naibu waziri wa nishati na madini Mhe. Dk. Medard Kalemani ameliagiza shirika la ugavi wa umeme nchini (TANESCO ) mkoani Mwanza kuhakikisha kuwa wateja ambao bado hawajaunganishiwa huduma hiyo, wanapatiwa umeme mara moja kabla ya julai 25 mwaka huu.

Dk. Kalemani ametoa agizo hilo wakati akizindua mradi wa kusambaza umeme vijijini ( REA ) awamu ya tatu katika mkoa wa Mwanza uliofanyika katika kijiji cha Nyamatala kata ya Ngulla wilayani Kwimba.

Mkurugenzi mkuu wa wakala wa umeme vijijini Mhandisi Gissima Nyamhanga, anasema mkandarasi wa mradi huo white city international inayoshirikiana na kampuni ya kichina iitwayo Gwadongi imepangiwa kutekeleza mradi huo katika vijiji 152 katika awamu ya kwanza inayoanza sasa hadi machi 2019.

Baadhi ya wabunge wa mkoa wa Mwanza, wakiongozwa na mbunge wa jimbo la Sumve Mhe. Richard Ndassa wamezungumzia changamoto za upatikanaji wa umeme zinazowakabili wananchi wa vijijini,

Aidha  mkuu wa mkoa huo John Mongella amesema kuwa  wakuu wa wilaya na wakurugenzi watendaji wa halmashauri za wilaya juu wanatakiwa kusimamia  mradi huo.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu