Naibu waziri wa nishati na madini aagiza wateja mkoani Mwanza wafungie umeme kabla ya julai 25.

In Kitaifa

Naibu waziri wa nishati na madini Mhe. Dk. Medard Kalemani ameliagiza shirika la ugavi wa umeme nchini (TANESCO ) mkoani Mwanza kuhakikisha kuwa wateja ambao bado hawajaunganishiwa huduma hiyo, wanapatiwa umeme mara moja kabla ya julai 25 mwaka huu.

Dk. Kalemani ametoa agizo hilo wakati akizindua mradi wa kusambaza umeme vijijini ( REA ) awamu ya tatu katika mkoa wa Mwanza uliofanyika katika kijiji cha Nyamatala kata ya Ngulla wilayani Kwimba.

Mkurugenzi mkuu wa wakala wa umeme vijijini Mhandisi Gissima Nyamhanga, anasema mkandarasi wa mradi huo white city international inayoshirikiana na kampuni ya kichina iitwayo Gwadongi imepangiwa kutekeleza mradi huo katika vijiji 152 katika awamu ya kwanza inayoanza sasa hadi machi 2019.

Baadhi ya wabunge wa mkoa wa Mwanza, wakiongozwa na mbunge wa jimbo la Sumve Mhe. Richard Ndassa wamezungumzia changamoto za upatikanaji wa umeme zinazowakabili wananchi wa vijijini,

Aidha  mkuu wa mkoa huo John Mongella amesema kuwa  wakuu wa wilaya na wakurugenzi watendaji wa halmashauri za wilaya juu wanatakiwa kusimamia  mradi huo.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu