Nape: Nitashugulika na CCM bila kutoka.

In Kitaifa, Siasa

Mbunge wa Jimbo la Mtama (CCM) Nape Nnauye amesema kuwa tetesi zilizokuwa zikizagaa na kuzungumzwa kuwa naye yuko mbioni kuhama chama chake cha mapinduzi kama ambavyo amefanya Lazaro Nyalandu.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram amepost picha wakiwa watatu akiwemo yeye, Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana, na aliyekuwa Mbunge kupitia CCM ambaye amejivua uanachama Lazaro Nyalandu.

Aidha Nape ameandika maneno ambayo yanaonyesha hana mpango wa kuhama chama chake kama ambavyo inahisiwa na watu mbali mbali, lakini akasema atainyoosha CCM akiwa ndani ya chama hicho.

“Chama cha siasa ni itikadi, itikadi ni imani.Siamini sana katika kubadili imani kienyeji.Nitashughulikia mapungufu nikiwa ndani na sio nje ili kukiweka sawa chama kinapoyumba na si vingine,”ameandika Nape
Kufuatia kuonyesha msimamo huo, hii moja kwa moja itafunga majadiliano ya watu katika sehemu tofauti kuwa ana mpango wa kukitosa Chama cha Mapinduzi c CCM.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu