NATO yatishia kuishambulia Korea Kaskazini.

In Kimataifa

 

 

Katibu Mkuu wa Shirika la kujihami la nchi za magharibi NATO Jens Stoltenberg, amesema mpango wa nyuklia wa Korea Kaskazini ni tisho kwa usalama wa dunia nzima, na kama zisipochukuliwa hatua stahiki basi kuna uwezekano wa kuleta madhara makubwa.

Amesema katika sheria ambazo shirika limejiwekea, ni pamoja na ile inayosema kuwa mwanachama mmoja akishambuliwa basi itakuwa limeshambuliwa shirika zima, hivyo kutanabaisha kwa kile kinachoendelea Korea Kaskazini.

Aidha alipoulizwa kama shirika hilo lina mpango wa kuishambulia Korea Kaskazini amesema kuwa, hana uhakika kama watatumia sheria hiyo, inayosema mwanachama mmoja akishambuliwa basi shirika zima limeshambuliwa.

Hata hivyo ametoa wito kwa Korea Kaskazini kuacha mpango wake wa kutengeneza silaha za nyuklia, huku akisema kufanya hivyo ni ukiukwaji mkubwa wa maazimio ya Umoja wa Mataifa na ni tishio kwa amani ya dunia.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu