NATO yatishia kuishambulia Korea Kaskazini.

In Kimataifa

 

 

Katibu Mkuu wa Shirika la kujihami la nchi za magharibi NATO Jens Stoltenberg, amesema mpango wa nyuklia wa Korea Kaskazini ni tisho kwa usalama wa dunia nzima, na kama zisipochukuliwa hatua stahiki basi kuna uwezekano wa kuleta madhara makubwa.

Amesema katika sheria ambazo shirika limejiwekea, ni pamoja na ile inayosema kuwa mwanachama mmoja akishambuliwa basi itakuwa limeshambuliwa shirika zima, hivyo kutanabaisha kwa kile kinachoendelea Korea Kaskazini.

Aidha alipoulizwa kama shirika hilo lina mpango wa kuishambulia Korea Kaskazini amesema kuwa, hana uhakika kama watatumia sheria hiyo, inayosema mwanachama mmoja akishambuliwa basi shirika zima limeshambuliwa.

Hata hivyo ametoa wito kwa Korea Kaskazini kuacha mpango wake wa kutengeneza silaha za nyuklia, huku akisema kufanya hivyo ni ukiukwaji mkubwa wa maazimio ya Umoja wa Mataifa na ni tishio kwa amani ya dunia.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

NACTIVET YASIMAMISHA MAFUNZO CHUO CHA MBEYA TRAINING..DC MALISA AAGIZA KUFANYIWA UHAKIKI VYUO VYOTE WILAYA YA MBEYA

Wazazi Wanafunzi na wahitimu wa chuo cha Mbeya training wameiomba serikali iwasaidie kurudishiwa stahiki zao mara baada ya kubainika

Read More...

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMANNE NOVEMBA 7, 2023

Manchester United na Newcastle United zote zinamfuatilia mshambuliaji wa Lyon Mfaransa Rayan Cherki, 20, ambaye mkataba wake unamalizika Juni

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu