NATO yatishia kuishambulia Korea Kaskazini.

In Kimataifa

 

 

Katibu Mkuu wa Shirika la kujihami la nchi za magharibi NATO Jens Stoltenberg, amesema mpango wa nyuklia wa Korea Kaskazini ni tisho kwa usalama wa dunia nzima, na kama zisipochukuliwa hatua stahiki basi kuna uwezekano wa kuleta madhara makubwa.

Amesema katika sheria ambazo shirika limejiwekea, ni pamoja na ile inayosema kuwa mwanachama mmoja akishambuliwa basi itakuwa limeshambuliwa shirika zima, hivyo kutanabaisha kwa kile kinachoendelea Korea Kaskazini.

Aidha alipoulizwa kama shirika hilo lina mpango wa kuishambulia Korea Kaskazini amesema kuwa, hana uhakika kama watatumia sheria hiyo, inayosema mwanachama mmoja akishambuliwa basi shirika zima limeshambuliwa.

Hata hivyo ametoa wito kwa Korea Kaskazini kuacha mpango wake wa kutengeneza silaha za nyuklia, huku akisema kufanya hivyo ni ukiukwaji mkubwa wa maazimio ya Umoja wa Mataifa na ni tishio kwa amani ya dunia.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Maagizo ya wizara kuhusu mfuko wa maendeleo ya kilimo.

Naibu Waziri Wa Kilimo Anthony Mavunde, amesema serikaliimeanza kutekeleza uanzishwaji wa mfuko wa maendeleo yakilimo utakaosaidia kukabiliana na changamoto

Read More...

TANZIA: WAZIRI MSTAAFU WA KILIMO AFARIKI DUNIA

Aliyewahi kuwa mbunge wa jimbo la Musoma Vijijini na Waziri wa Kilimo na Mifugo Mhe. Herman Kirigini Amefariki Dunia. Akithibitisha

Read More...

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Professor Makame Mbarawaameliomba Bunge kumuidhinishia kiasi cha Sh Trilioni 3.6ikiwa ni makadirio ya mapato

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu