Nchi ya Qatar imefungua huduma za usafiri wa meli kutokea Oman kwa lengo la kukabiliana na vikwazo vya usafiri vilivyowekwa na majirani zake.

Nchi ya Qatar imefungua huduma za usafiri wa meli kutokea Oman kwa lengo la kukabiliana na vikwazo vya usafiri vilivyowekwa na majirani zake.

Meli kadhaa zikiwa zimebeba vyakula na bidhaa mbalimbali zimeonekana zikielekea Qatar kutokea bandari mbili zilizopo Oman.

Qatar inategemea uingizwaji wa chakula kutoka nje.

Saudi Arabia, Bahrain na muungano wa Falme za Kiarabu zilizuia uingizwaji wa bidhaa kwenda Qatar wiki chache zilizopita kwa shutuma kuwa nchi hiyo inaunga mkono vitendo vya kigaidi.

Waziri wa mambo ya nje wa Qatar amewasili mjini London na kisha Paris kujadili mgogoro huo.

 

Exit mobile version