Ndalichako asema uhakiki wa vyeti feki ulifanyika kwa umakini na kwa uhakika ili kutenda haki.

In Kitaifa

WAZIRI wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo wa Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako amesema uhakiki wa vyeti feki ulifanyika kwa umakini na kwa uhakika ili kutenda haki.

Ripoti iliyokabidhiwa kwa Rais John Magufuli na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Angela Kairuki, ilikuwa na orodha ya watumishi wa umma 9,932 walionainika kuwa na vyeti feki. Profesa Ndalichako alisema hadi kufikia kuwaweka wazi, ulifanyika uchunguzi wa kina na makini.

Amesema baada ya uhakiki huo uliojikita katika vyeti vya kidato cha nne, kidato cha sita na ualimu, zamu inayofuata ni uhakiki wa vya kitaaluma baada ya kukamilika kwa uhakiki wa watumishi wa Serikali Kuu utakaotangazwa wiki hii.

Amesema Serikali imeziba njia zote za mkato katika elimu na ajira hivyo, vijana watumie muda walio nao kusaoma kwa bidii. Aliwataka waliojiunga katika vyuo vikuu bila sifa stahiki kuwajisalimishe ili kuepuka majuto ya baadaye.

Profesa Ndalichako alisema suala la kughushi vyeti vya taaluma na kutumia vya wengine limekuwa changamoto kubwa nchini.

Ndalichako amesema  serikali ina dhamira ya kuhakikisha watumishi wenye sifa stahiki wanakuwepo kwenye utumishi wa umma na si vinginevyo na kwamba, Mei 5, mwaka huu Serikali itatoa taarifa ya uhakiki wa watumishi wa Serikali Kuu.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu