Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Abeid Aman Karume
visiwani Zanzibar umeendelea kupokea ndege ya shirika al
Qatar Air aina ya Dreamliner 787 iliyobeba watalii zaidi ya 80
kutoka Doha nchini Qatar.
Leo ndege ya Qatar imetua katika uwanja wa kimataifa wa KIA
ikiwa na watalii 50 kutoka nchi mbalimbali ambao wamefika
nchini Tanzania kwa ajili yakutembelea hifadhi za taifa ambapo
ni miezi minne imepita baada yakuwepo kwa changamoto ya
ugonjwa wa Corona nakupelekea nchi nyingi kusitisha safari
zake.