NEC yaelezwa jimbo la Singida Kaskazini liko wazi.

In Kitaifa, Siasa

Spika wa Bunge Job Ndugai ametangaza kuwa jimbo la Singida Kaskazini lililokuwa likishilikiwa na Lazaro Nyalandu liko wazi baada ya mbunge huyo kufutwa uanachama na CCM.
Taarifa iliyotolewa leo na Ofisi ya Bunge imeeleza kuwa, Spika Ndugai amemuandikia Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi NEC Jaji Semistocles Kaijage kumfahamisha kuwa jimbo hilo liko wazi.
Kwa mujibu wa kifungu 37 (3) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi 2015 kinaeleza kwamba, pale mbunge atajiuzulu, atakufa au sababu nyingine yeyote tofauti na zilizoainishwa katika kifungu cha 113, Spika atamjulisha Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi na kutangaza kwenye Gazeti la Serikali, kwamba kiti hicho cha ubunge kiko wazi.
Kufuatia barua hiyo Tume ya Taifa ya Uchaguzi inaweza kuendelea na mchakato wa kumpata mbunge wa kujaza nafasi hiyo iliyo wazi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu