NEC yaruhusu leseni ya udereva kupigia kura.

In Kitaifa

Kwa mujibu wa kifungu cha 62 (a) sheria ya Uchaguzi wa Seriakli za mtaaa, Tume ya uchaguzi imeruhusu wapigakura walipoteza vitambulisho vya kupigia kura kupata fursa ya kushiriki zoezi hilo kwenye uchaguzi mdogo wa madiwani wa kata 43.

Ambapo imesema katika Uchaguzi huo unaotarajiwa kufanyika rasmi Novemba 26 wapiga kura wameruhusiwa kupiga kura kwa kutumia leseni zao za udereva, pasi ya kusafiria pamoja na vitambulisho vya uraia vianvyotolewa na Mamlaka ya Vitambulsho vya Taifa NIDA.

Fursa hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi NEC, Ramadhani Kailima alipokuwa akitoa mafunzo ya siku tatu kwa wasimamizi wa uchaguzi huo.

Aidha amefafanua kuwa ruhusa hiyo imetolewa kwa sharti la kwamba majina na herufi yaliyopo kwenye kitambulisho hicho yafanane na majina na herufi zilizopo kwenye Daftari la kudumu la wapiga kura.

Hata hivyo Mafunzo hayo bado yanaendelea kufanyika jijini Dodoma kuwaandaa wasimamizi wa uchaguzi huo.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu