NEC yaruhusu leseni ya udereva kupigia kura.

In Kitaifa

Kwa mujibu wa kifungu cha 62 (a) sheria ya Uchaguzi wa Seriakli za mtaaa, Tume ya uchaguzi imeruhusu wapigakura walipoteza vitambulisho vya kupigia kura kupata fursa ya kushiriki zoezi hilo kwenye uchaguzi mdogo wa madiwani wa kata 43.

Ambapo imesema katika Uchaguzi huo unaotarajiwa kufanyika rasmi Novemba 26 wapiga kura wameruhusiwa kupiga kura kwa kutumia leseni zao za udereva, pasi ya kusafiria pamoja na vitambulisho vya uraia vianvyotolewa na Mamlaka ya Vitambulsho vya Taifa NIDA.

Fursa hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi NEC, Ramadhani Kailima alipokuwa akitoa mafunzo ya siku tatu kwa wasimamizi wa uchaguzi huo.

Aidha amefafanua kuwa ruhusa hiyo imetolewa kwa sharti la kwamba majina na herufi yaliyopo kwenye kitambulisho hicho yafanane na majina na herufi zilizopo kwenye Daftari la kudumu la wapiga kura.

Hata hivyo Mafunzo hayo bado yanaendelea kufanyika jijini Dodoma kuwaandaa wasimamizi wa uchaguzi huo.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu