Nimeota Lulu ataachiwa huru.

Baba mzazi wa Marehemu Steven Kanumba anayefahamika kwa jina la Charles Kanumba amesema kuwa ameota ndoto kuhusu maamuzi ya Mahakama dhidi ya Elizabeth Michael maarufu kama Lulu.

Baba Kanumba amesema kuwa amekuwa akioteshwa kuhusu uamuzi wa Mahakama na kwamba aliota Lulu ataachiwa huru.

Ameeleza kuwa kwa kifungo cha miaka miwili kwa kosa hilo ni adhabu ndoto inayofanana na ndoto yake ya kuachiwa huru. Hata hivyo, amesema kwakuwa amesikia mawakili wanaomtetea Lulu watakata rufaa dhidi ya hukumu hiyo, anaamini ndoto yake itatimia kwani ataachiwa huru.

“Nimekuwa naoteshwa, na kila nachokiota kinakuwa kweli. Nimesikia wanakata rufaa, na wakikata rufaa lazima Lulu ataachiwa. Nimeshaoteshwa kuhusu hilo,” Baba Kanumba ameiambia Amplifaya ya Clouds FM.

Exit mobile version