Nyalandu asema sababu za kuelekea Chadema.

In Kitaifa, Siasa

Aliyekuwa mbunge wa Kigoma Kaskazini CCM Lazaro Nyalandu, amesema ni kwa nini ameamua kutaka kujiunga chadema na sio chama kingine cha siasa hapa nchini.
Nyalandu ambaye amewahi kuwa naibu waziri wa Wizara ya Viwanda na Biashara na baadaye Maliasili na Utalii kabla ya kuwa waziri kamili, alitangaza uamuzi wa kuhama CCM Jumatatu.
Moja ya sababu alizozieleza ni kutoridhishwi na mwenendo wa kisiasa nchini, ukiukwaji wa haki za binadamu, dhuluma na mihimili miwili ya nchi kushindwa kufanya kazi yake kwa uhuru.
Amesema kuhama CCM ni kitu kilichomchukua muda mrefu, kutokana na yanayoendelea ndani ya chama hicho tawala,na hapa anaeleza kwa nini ameamua kuelekea CHADEMA.

Pia Nyalandu amesema uamuzi wake wa kujitoa CCM ni moja ya mambo matatu makubwa aliyofanya maishani hadi sasa.
Uamuzi wa kwanza ukiwa ni wa kumfuata Yesu Kristo awe mwokozi wa maisha yake, wa pili kuamua mwanamke gani awe mke wake na watatu ni huo wa kuamua kuachana na CCM.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu