Nyalandu Ngoma nzito.

In Kitaifa

Kashfa zinazomkabili  aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu zimetua mikononi mwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kwa ajili ya uchunguzi.

Nyalandu anadaiwa kutumia ofisi vibaya na kuisababishia serikali hasara ya shilingi bilioni 32, katika kipindi cha miaka miwili alichoongoza wizara hiyo kuanzia mwaka 2014 hadi 2015.

Aidha, uchunguzi huo umejiri zikiwa zimepita siku 21 tangu Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamis Kigwangalla kulieleza bunge kuhusu kashfa tatu za ubadhirifu zinazomkabili Lazaro Nyalandu.

Katika mkutano huo wa bunge, Dkt. Kigwangallah alivitaka vyombo vya usalama ikiwemo polisi na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kufanya uchunguzi wa tuhuma hizo.

“Uchunguzi unaendelea, tunakamilisha vielelezo vikikamilika hatua nyingine zitafuata, lakini ninahakikisha tunafanya hivyo, siwezi kusema sana wala kulizungumzia kiundani zaaidi kwa sababu za kiupelelezi,”amesema Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Valentino Mlowola.

Hata hivyo, Dkt. Kigwangalla alizitaja tuhuma zinazomkabili Nyalandu kuwa ni pamoja na ile ya kukodisha chumba kwenye hoteli ya Serena iliyogharimu kiasi cha shilingi bilioni 16 lakini hakusaini mapendekezo mpaka alipotoka madarakani, kashfa ya pili iliyotajwa na waziri huyo ni ile ya kugawa vitalu zaidi ya vitano kwa kampuni za Mwiba Holdings, Wingetwindlos na Tanzania Game Trackers Safari zinazomilikiwa na bilionea kutoka Marekani, huku kashfa ya tatu ikiwa ni ile ya kutumia Helkopta ya kukodi wakati wa kuwania kugombea nafasi ya Urais.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu