Mchakato wa ujenzi wa nyumba 47 za wakazi wa maeneo
yanayozunguka Mgodi Williamson Diamond Ltd, ambao
nyumba na mashamba yao yaliathirika baada ya bwawa la
kuhifadhia tope kuvunjika kingo, umekamilika.
Aidha Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Christina Mndeme
ameagiza uongozi wa mgodi huo kukamikisha ujenzi wa bwawa
jipya la maji tope mwezi Julai, na kuanza uzalishaji wa almasi
ambao ulisimama tangu mwezi wa 11 mwaka jana.