Ofisi ya Waziri Mkuu wa Uingereza Theresa May leo Jumapili imesema kuwa mazungumzo yanaendelea na chama cha DUP katika kutafuta uungaji mkono wake kwa ajili ya kuunda serikali baada ya kusema mapema kuwa makubaliano yalikuwa yamefikiwa.

In Kimataifa
Ofisi ya Waziri Mkuu wa Uingereza Theresa May leo Jumapili imesema kuwa mazungumzo yanaendelea na chama cha DUP katika kutafuta uungaji mkono wake kwa ajili ya kuunda serikali baada ya kusema mapema kuwa makubaliano yalikuwa yamefikiwa.
Chama cha Conservative cha waziri mkuu May kilipoteza viti vya wabunge wengi katika uchaguzi wa mapema siku ya Alhamisi na sasa kinahitaji msaada wa wabunge 10 kutoka chama cha DUP jambo linalozua wito kumtaka ajiuzulu.
Hapo jana May alilazimika kuwaachia wasaidizi wake wawili wa karibu baada ya kupata ugumu katika kuimarisha mamlaka yake kufuatia kushindwa kupata idadi kubwa ya wabunge katika uchaguzi huo.
Aidha Viongozi wakuu wa chama wameonya dhidi ya mabadiliko ya haraka ya uongozi wakisema kuwa yatasababisha usumbufu zaidi wakati huu Uingereza ikijiandaa kuanza mazungumzo ya kujiondoa kwenye umoja wa Ulaya mapema tarehe 19 Juni.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu