Paka Mwizi Anaswa Akiiba Vitu vya Majirani.

In Kimataifa

Paka mmoja nchini Uingereza aliyekuwa na mazoea ya kuiba
nguo na chakula mara kwa mara kutoka kwa majirani
amenaswa.


Mmiliki wa paka huyo Donna Hibbert, akiwa amejawa na soni,
ameingia kwenye mtandao wa Facebook akijaribu kurudisha
vitu hivyo.


Paka huyo kwa jina Harry, anaripotiwa kwamba amekuwa
akipeleka nyumbani mara kwa mara bidhaa zilizoibwa ikiwa ni

pamoja na nguo za ndani, pakiti ya soseji na hata kiatu cha
wabunifu katika kipindi cha miaka minne iliyopita.


Kulingana na Hibbert katika wiki moja iliyopita, Harry
alichukua vitu sita kutoka kwa majirani akifikiria ni zawadi.
Baadhi ya vitu hivyo vimechukuliwa kutoka kweny kamba za
kuanikia nguo,lakini vingine vimechukuliwa kutoka ndani ya
nyumba za watu.


Kaka yake Harry anaitwa Luna pia ni ,lakini kwa kawaida
huchukua vitu kama vile pakiti nyororo na pakiti za sigara.


Hibbert sasa ameanza kuchapisha vitu vilivyoibiwa kwenye
ukurasa wa Facebook wa Spotted,ambapo hata jirani wake wa
karibu ameweza kutambua vitu vyake.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu