Papa Francis akutana na waathirika wa unyanyasaji wa kingono katika mkutano wa vijana katoliki duniani

In Kimataifa

Papa Francis Jumatano alisema kanisa katoliki linahitaji “kujitakasa kwa unyenyekevu na kwa muda mrefu” ili kukabiliana na “kilio cha uchungu” cha waathirika wa unyanyasaji wa kingono waliotendewa na makasisi.

Alikutana na waathirika hao kwa faragha jana Jumatano katika siku ya kwanza ya ziara yake nchini Ureno.

Francis alikuwa akizungumza mjini Lisbon mwanzoni mwa ziara ya siku tano nchini humo ambayo anatumai itawahamasisha vijana wa kikatoliki wakati wa siku ya vijana duniani, tamasha kubwa zaidi la kikatoliki duniani.

Miezi sita iliyopita, ripoti ya tume ya Ureno ilisema takriban watoto 4,815 walinyanyaswa kingono na makasisi kwa zaidi ya miongo saba.

Mzozo huu “unatuomba kujitakasa kwa unyenyekevu kwa muda mrefu, tukianza na kilio cha uchungu cha waathirika, ambao lazima wakubaliwe na wasikilizwe kila mara,” Francis alisema katika hotuba yake kwa maaskofu, mapadre na watawa katika ibada ya jioni ndani ya makazi ya watawa.

Francis alikutana kwa faragha na waathirika 13 walionyanyaswa kingono katika ubalozi wa Vatican mjini Lisbon jana Jumatano jioni, huku Vatican ikisema katika taarifa kwamba mkutano huo ulifanyika katika “mazingira ya usikilizaji mkubwa” na ulidumu kwa zaidi ya saa moja.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu