Papa Francis atoa wito na kukataa ushabiki ili kuimarisha maridhiano na waislamu na kuwaunga mkono wakristo wachache nchini Misri.

In Kimataifa

Kiongozi wa kanisa katoliki duniani Papa Francis amekataa ushabiki na kutoa wito wa upendo katika misa iliyofurahiwa na umati wa maelfu ya Wakatoliki wa Misri wakati wa ziara inayolenga kuimarisha maridhiano na waislmu na kuwaunga mkono wakristo wachache nchini humo.

Ziara hiyo inayofanyika baada ya kundi la Islamic State kuwaua waumini kadhaa katika mashambulizi matatu kwenye makanisa mwezi Desemba mwaka jana na Aprili mwaka huu, imewapa wakristo hao wenye mazingira magumu ya kuabudu fursa ya kusherehekea.

Papa Francis amewaambia waumini kuwa ushabiki ambao waumini wanapaswa kuwa nao ni ushabiki wa upendo na ushabiki mwingine hautoki kwa Mungu.

Kiongozi huyo wa kiroho kwa karibu wakatoliki bilioni 1.3 duniani anakuwa papa wa kwanza kutembelea makao makuu ya imam mkuu wa Al-Azhar, Ahmed al-Tayeb, mmoja wa viongozi wa malaka ya juu ya kiislamu duniani.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu