Papa Francis atoa wito na kukataa ushabiki ili kuimarisha maridhiano na waislamu na kuwaunga mkono wakristo wachache nchini Misri.

In Kimataifa

Kiongozi wa kanisa katoliki duniani Papa Francis amekataa ushabiki na kutoa wito wa upendo katika misa iliyofurahiwa na umati wa maelfu ya Wakatoliki wa Misri wakati wa ziara inayolenga kuimarisha maridhiano na waislmu na kuwaunga mkono wakristo wachache nchini humo.

Ziara hiyo inayofanyika baada ya kundi la Islamic State kuwaua waumini kadhaa katika mashambulizi matatu kwenye makanisa mwezi Desemba mwaka jana na Aprili mwaka huu, imewapa wakristo hao wenye mazingira magumu ya kuabudu fursa ya kusherehekea.

Papa Francis amewaambia waumini kuwa ushabiki ambao waumini wanapaswa kuwa nao ni ushabiki wa upendo na ushabiki mwingine hautoki kwa Mungu.

Kiongozi huyo wa kiroho kwa karibu wakatoliki bilioni 1.3 duniani anakuwa papa wa kwanza kutembelea makao makuu ya imam mkuu wa Al-Azhar, Ahmed al-Tayeb, mmoja wa viongozi wa malaka ya juu ya kiislamu duniani.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu