Papa Francis atoa wito na kukataa ushabiki ili kuimarisha maridhiano na waislamu na kuwaunga mkono wakristo wachache nchini Misri.

In Kimataifa

Kiongozi wa kanisa katoliki duniani Papa Francis amekataa ushabiki na kutoa wito wa upendo katika misa iliyofurahiwa na umati wa maelfu ya Wakatoliki wa Misri wakati wa ziara inayolenga kuimarisha maridhiano na waislmu na kuwaunga mkono wakristo wachache nchini humo.

Ziara hiyo inayofanyika baada ya kundi la Islamic State kuwaua waumini kadhaa katika mashambulizi matatu kwenye makanisa mwezi Desemba mwaka jana na Aprili mwaka huu, imewapa wakristo hao wenye mazingira magumu ya kuabudu fursa ya kusherehekea.

Papa Francis amewaambia waumini kuwa ushabiki ambao waumini wanapaswa kuwa nao ni ushabiki wa upendo na ushabiki mwingine hautoki kwa Mungu.

Kiongozi huyo wa kiroho kwa karibu wakatoliki bilioni 1.3 duniani anakuwa papa wa kwanza kutembelea makao makuu ya imam mkuu wa Al-Azhar, Ahmed al-Tayeb, mmoja wa viongozi wa malaka ya juu ya kiislamu duniani.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu