Peter Crouch aingia kwenye kitabu cha rekodi za dunia.

In Kimataifa, Michezo

Mshambuliaji wa klabu ya Stoke ya Uingereza Peter Crouch, ameingizwa kwenye kitambu cha rekodi za dunia cha Guinness World Records cha mwaka 2018 kwa kufunga mabao mengi zaidi kwa kichwa Ligi ya Uingereza.

Crouch amefunga mabao 51 kwa kichwa katika ligi hiyo, mabao matano zaidi ya mshambuliaji wa zamani wa Blackburn na Newcastle Alan Shearer.

Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 36 amefunga jumla ya mabao 105 katika ligi kuu ya Uingereza katika mechi 436 alizochezea jumla ya klabu sita ligi hiyo.

Crouch alifunga bao la ushindi mechi ya karibuni zaidi ya Stoke walipocheza dhidi ya Southampton katika ligi kuu ya Uingereza.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu