Picha za mateso ya mwanasiasa aliyewekwa kizuizini akiwa na majeraha mwilini mwake.

In Kimataifa

Nchini Uganda picha zinazomuonesha meya wa mji mdogo magharibi mwa nchi hiyo,Geoffrey Byamukama, akiwa amelazwa juu ya kitanda cha hospitali akionekana na majeraha katika magoti na vifundo vya miguu ,vilivyovimba pamoja na michubuko mahali pengine kwenye mwili wake, zilisambaa katika mitandao ya kijamii na vyombo vya habari vya ndani ya nchi siku ya Alhamisi.

Watetezi wa haki za binaadamu nchini humo wanasema picha hizo za mateso za mwanasiasa aliyewekwa kizuizini, akiwa na majeraha mwilini mwake, zinaonyesha ukatili wa kutojali unaofanywa na maafisa wa usalama nchini humo.

Idara ya usalama chini Uganda inakana kutumia mateso kama njia ya kupata ushahidi, kutoka kwa watuhumiwa waliowakamata.Msemaji wa polisi Asan Kasingye amesema maafisa wawili wa usalama wamekamatwa kuhusiana na mateso ya Byamukama lakini hakutoa maelezo zaidi.

Kasingye ameliambia shirika la habari la Reuters kwamba hawafumbii macho mateso na kwamba huo sio utaratibu wao wa kazi.

Byamukama alikamatwa April 5 kwa tuhuma za kushiriki katika mauaji ya afisa wa polisi wa ngazi ya juu Andrew Felix Kaweesi, Machi 17.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu