Polepole asema ccm sasa ni chama cha wananchi wote.

In Kitaifa

KATIBU wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi, Itikadi na Uenezi, Humphrey Polepole amesema zama za watu wachache wenye fedha chafu, kuhonga wanachama na kuweka viongozi wanaowataka, zimekwisha.

Amesema CCM sasa ni chama cha wanachama wote kama Katiba inavyosema, bila ya kujali rika wala rangi na wenye kutaka uongozi ndani ya chama kwa kutumia fedha chafu, chama hakitasita kuwachukulia hatua ikiwamo kukata majina yao.

Kiongozi huyo wa CCM ameyasema hayo mkoani Arusha alipokutana na viongozi wa chama wa Wilaya ya Arusha ,kutoka kata zote 25 wakiwemo wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Wilaya ya Arusha.

Aidha amewataka wanaCCM kuwataja viongozi wanaotaka uongozi ,kwa kugawa fedha chafu ili hatua stahiki zichukuliwe dhidi yao.

Polepole amewataka wakazi wa Arusha kutorudia makosa yaliyojitokeza katika uchaguzi zilizopita.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu