Polepole asema ccm sasa ni chama cha wananchi wote.

In Kitaifa

KATIBU wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi, Itikadi na Uenezi, Humphrey Polepole amesema zama za watu wachache wenye fedha chafu, kuhonga wanachama na kuweka viongozi wanaowataka, zimekwisha.

Amesema CCM sasa ni chama cha wanachama wote kama Katiba inavyosema, bila ya kujali rika wala rangi na wenye kutaka uongozi ndani ya chama kwa kutumia fedha chafu, chama hakitasita kuwachukulia hatua ikiwamo kukata majina yao.

Kiongozi huyo wa CCM ameyasema hayo mkoani Arusha alipokutana na viongozi wa chama wa Wilaya ya Arusha ,kutoka kata zote 25 wakiwemo wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Wilaya ya Arusha.

Aidha amewataka wanaCCM kuwataja viongozi wanaotaka uongozi ,kwa kugawa fedha chafu ili hatua stahiki zichukuliwe dhidi yao.

Polepole amewataka wakazi wa Arusha kutorudia makosa yaliyojitokeza katika uchaguzi zilizopita.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu