Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es salaam limetangaza
Oparesheni kali ya kuwasaka kwa nguvu zote kikundi cha
Wahalifu zaidi 10 waliokuwa na Silaha za Jadi, ambao
walivamia nyumba moja iliyopo Kawe mzimuni kwa kuvunja
milango kisha kupora Fedha, Mali, kujeruhi watu watatu na
kusababisha kifo cha Mtu mmoja aliyetajwa kwa majina ya
Maria Pascal.
Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam
ACP William Mkonda amesema tukio hilo limetokea Septemba
14, 2022 majira ya Saa nane na nusu Usiku.
Amesema uhalifu huo ni tukio baya ambapo kila mtanzania
anapaswa kulani Unyama huo ambao hutumiwa na baadhi ya
watu wasiotaka kujipatia kipato chao kwa njia halali.