Polisi nchini Uganda imewakamata karibu watu 56 hapo jana kwa kuandaa mikutano ya hadhara kinyume cha sheria.

In Kimataifa
Polisi nchini Uganda imewakamata karibu watu 56 hapo jana kwa kuandaa mikutano ya hadhara kinyume cha sheria.
Wanaharakati waliingia mitaani kuupinga mpango wa serikali unaodai kuondoa ukomo wa umri kwa wagombea wa urais, ikiwa ni uwezekano wa kumwezesha Rais Yoweri Museveni ambaye ana umri wa miaka 72 kuendelea kuwa madarakani baada ya mwaka wa 2021.
Kwa sasa, katiba inawazuia raia wa zaidi ya umri wa miaka 75 kugombea wadhifa wa urais.
Maafisa wa upinzani wanalalamika kuhusu ukamataji huo, wakati pia wakiikosoa serikali kwa kuwakandamiza wapinzani wa mpango huo.
Museveni, ambaye amekuwa madarakani tangu mwaka wa 1986, aliwaambia waandishi wa habari kuwa hana ufahamu wa mpango huo unaoweza kuurefusha utawala wake.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu