Polisi nchini Uingereza wameyalaumu machapisho yaliyotolewa katika gazeti la New York Times juu ya picha na taarifa kutoka katika eneo ambalo shambulio la bomu lilitokea mjini Manchester.

In Kimataifa

Polisi nchini Uingereza wameyalaumu machapisho yaliyotolewa katika gazeti la New York Times juu ya picha na taarifa kutoka katika eneo ambalo shambulio la bomu lilitokea mjini Manchester.

Maafisa nchini humo wanasema kuvuja kwa picha hizo kuna haribu uchunguzi wa polisi na kuondoa imani na washirika wao katika masuala ya kiintelejinsia.

Picha hizo zinaonesha vitu mbalimbali ambavyo vingetumika kama ushahidi kama vile betri na vitu vingine vyenye muonekano wa vilipuzi.

Hata hivyo gazeti hilo la Marekani limejitetea juu ya picha hizo ambazo imesema zinaashiria kuwa bomu lililotumika katika shambulio hilo kwa kiasi kikubwa linaonekana kuwa ni la kisasa.

Waziri mkuu wa Uingereza anatarajiwa kulipeleka suala hilo kwa Rais wa Marekani Donald Trump wakati wa mkutano wa nchi wanachama wa Jumuia ya NATO, ambao unafanyika leo.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu