Polisi Rwanda wakanusha kumzuia mwanamke aliyetaka kuwania Urais.

In Kimataifa, Siasa

Polisi nchini Rwanda wamekanusha kwamba wanamzuilia mwanamke aliyetaka kuwania urais katika uchaguzi uliofanyika mapema mwaka huu.

Taarifa zilikuwa zimeenea mitandao ya kijamii nchini humo kwamba polisi wamemkamata Diane Shima Rwigara na mamake.

Msemaji wa Polisi ya Rwanda Theos Badege amewaambia waandishi wa habari  kuwa polisi walifanya upekuzi nyumbani kwake kama sehemu ya upelelezi wa mwanzo kuhusu makosa anayotuhumiwa yeye na familia yake ambayo ni pamoja na kosa la kughushi nyaraka na kukwepa kulipa kodi.

 

Taarifa zilikuwa zimesema kuwa watu wasiojulikana ambao walikuwa na silaha lakini walivalia mavazi ya kiraia walivamia nyumbani kwa mwanasiasa huyo mapema leo Jumatano.

 

Familia yake inasema kufikia sasa bado mwanamke huyo na mamake hawajulikani waliko.

Diane Rwigara alikataliwa kugombea kiti cha urais katika uchaguzi uliofanyika mapema mwezi huu ambapo Rais Paul Kagame alishinda kwa kura nyingi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu