Polisi Rwanda wakanusha kumzuia mwanamke aliyetaka kuwania Urais.

In Kimataifa, Siasa

Polisi nchini Rwanda wamekanusha kwamba wanamzuilia mwanamke aliyetaka kuwania urais katika uchaguzi uliofanyika mapema mwaka huu.

Taarifa zilikuwa zimeenea mitandao ya kijamii nchini humo kwamba polisi wamemkamata Diane Shima Rwigara na mamake.

Msemaji wa Polisi ya Rwanda Theos Badege amewaambia waandishi wa habari  kuwa polisi walifanya upekuzi nyumbani kwake kama sehemu ya upelelezi wa mwanzo kuhusu makosa anayotuhumiwa yeye na familia yake ambayo ni pamoja na kosa la kughushi nyaraka na kukwepa kulipa kodi.

 

Taarifa zilikuwa zimesema kuwa watu wasiojulikana ambao walikuwa na silaha lakini walivalia mavazi ya kiraia walivamia nyumbani kwa mwanasiasa huyo mapema leo Jumatano.

 

Familia yake inasema kufikia sasa bado mwanamke huyo na mamake hawajulikani waliko.

Diane Rwigara alikataliwa kugombea kiti cha urais katika uchaguzi uliofanyika mapema mwezi huu ambapo Rais Paul Kagame alishinda kwa kura nyingi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu