Polisi wakamata usafiri uliotumika kuutupa mwili Chiloba

In Kimataifa

Miongoni mwa waliokamatwa ni watoto wawili huku mshukiwa mkuu
Jackton Odhiambo akikiri kumuua mwanamitindo huyo kwa usaidizi wa
washirika wawili ambao bado hawajakamatwa.


Uchunguzi kuhusu mauaji ya mwanaharakati na mwanamitindo wa
LGBTQ umechukua sura mpya huku polisi wakiwakamata washukiwa
wengine watatu huku mshukiwa mkuu Jackton Odhiambo akikiri
kumuua mwanamitindo huyo.

Watatu hao walikamatwa Jumamosi kwa kubeba sanduku la chuma
ambalo mwili wa Chiloba ulipatikana.
watu watatu waliokamatwa ni watoto wawili na mwanamume mmoja
ambaye polisi wanaamini kuwa anaweza kutoa taarifa muhimu kuhusu
mauaji hayo yaliyotikisa taifa.


Msemaji wa polisi Resla Onyango alithibitisha kuwa maafisa wa
upelelezi pia wamekamata gari linaloaminika kubeba maiti ya
mwanaharakati huyo hadi ilipotupwa.


Katika ungamo la kutisha, mshukiwa alifichua kwamba alimuua
mwanaharakati na mwanamitindo wa LGBTQ kwa usaidizi wa marafiki
wawili ambao bado hawajafahamika.

Jackton pia alifichua kuwa walikuwa kwenye uhusiano na waliishi
pamoja na marehemu kama mume na mke.
Mshukiwa huyo aliyejikiri aliongezea kuwa alimuua Chiloba kama
kulipiza kisasi kwa kumsaliti katika uhusiano wao.

OCPD wa Langas John Odhiambo alibainisha kuwa msako umeanzishwa
ili kuwapata washirika wawili wa Jackton ambao bado hawajapatikana.
Majirani walivutiwa na harufu mbaya iliyokuwa ikitoka katika nyumba
hiyo ambayo mshukiwa mkuu alishirikiana na marehemu.

“Aliwaambia majirani ni panya aliyekufa ambaye alikuwa ananuka
walipotafuta kujua nini kilikuwa kinanukia kutoka kwa nyumba

waliyokuwa wakiishi,” mkuu wa DCI kaunti ya Uasin Gishu Peter
Kimulwo alisema.

Majirani waliambia polisi kwamba walimwona Jackton akiwa na
sanduku la chuma siku moja kabla ya mwili wa Chiloba kupatikana
kwenye sanduku la chuma ambalo lilitupwa Halingham karibu na
Kipkaren.

Msimamizi wa nyumba aliyokuwa akiishi chiloba amby anafahamika
kwa jina la alex nyamwea amefichua kuwa rafiki yake ambaye ni
mshukiwa mkuu katika mauaji ya chiloba alihama kutoka nyumba hiyo
tarehe 4 mwezi huu na alimpgia simu kupitia simu ya marehemu
kumfahamisha kuwa ana hama.


Na baada ya mwili wa marehemu kukutwa umetupwa tarehe 3 mwezi
huu mshukiwa alionekana akibeba vyombo vya nyumba na kuhama
hapo walipokuwa wakiishi pamoja na kwa mujibu wa msimamizi wa
nyumba hizo mshukiwa huyo alionekana akiisafisha nyumba hyo

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

NACTIVET YASIMAMISHA MAFUNZO CHUO CHA MBEYA TRAINING..DC MALISA AAGIZA KUFANYIWA UHAKIKI VYUO VYOTE WILAYA YA MBEYA

Wazazi Wanafunzi na wahitimu wa chuo cha Mbeya training wameiomba serikali iwasaidie kurudishiwa stahiki zao mara baada ya kubainika

Read More...

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMANNE NOVEMBA 7, 2023

Manchester United na Newcastle United zote zinamfuatilia mshambuliaji wa Lyon Mfaransa Rayan Cherki, 20, ambaye mkataba wake unamalizika Juni

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu