PSG usiku wa kuamkia leo imefanikiwa kushinda kwa mabao 3-
0 dhidi ya Leipzig mjini Lisbon.
Mchezo huo wa hatua ya nusu fainali ulikuwa na ushindani
mkubwa na mwisho wa siku PSG wakaibuka wababe na kutinga
mazima hatua ya fainali.
Kipindi cha Kwanza PSG ilitupia mabao mawili ambapo bao la
kwanza lilipachikwa na Marquinhos dakika ya 13 na Di Maria
alifunga bao la pili dakika ya 42 na bao la tatu na la mwisho
lilipachikwa na Benatti dakika ya 56.
Fainali ya mchezo huo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya inatarajiwa
kuchezwa Jumapili, Agosti 23 na mshindi kati ya mchezo wa
Bayern Munich na Lyon.