PUTIN AUFUTA MKUTANO WA KILA MWAKA NA WAANDISHI WA HABARI

In Kimataifa

Rais wa Russia Vladimir Putin amefutilia mbali mkutano wa waandishi wa habari kama ilivyo kawaida yake kila mwisho wa mwaka, ikiwa ni mara ya kwanza kutofanya hivyo katika muda wa muongo mzima.

Kama ilivyo desturi, kikao cha Putin na waandishi wa habari huchukua saa kadhaa na kimekuwa sehemu ya shughuli za putin katika kalenda ya kila mwaka ambapo huwa anajibu maswali kutoka kwa waandishi wa habari wa ndani na wa kimataifa.

Msemaji wa Kremlin Dmitry Peskov, amewaambia waandishi wa habari kwamba kikao hicho cha habari cha kufunga mwaka, hakitafanyika bila kutaja sababu ambazo zimepelekea kikao hicho kutofanyika.

Peskov hata hivyo amesema kwamba Putin amekuwa akizungumza na waandishi wa habari kila mara, ikiwemo anapotembelewa na viongozi kutoka nchi nyingine, na kwamba kiongozi huyo wa Russia atapata fursa nyingine ya kuzungumza na waandishi wa habari.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu