PUTIN AUFUTA MKUTANO WA KILA MWAKA NA WAANDISHI WA HABARI

In Kimataifa

Rais wa Russia Vladimir Putin amefutilia mbali mkutano wa waandishi wa habari kama ilivyo kawaida yake kila mwisho wa mwaka, ikiwa ni mara ya kwanza kutofanya hivyo katika muda wa muongo mzima.

Kama ilivyo desturi, kikao cha Putin na waandishi wa habari huchukua saa kadhaa na kimekuwa sehemu ya shughuli za putin katika kalenda ya kila mwaka ambapo huwa anajibu maswali kutoka kwa waandishi wa habari wa ndani na wa kimataifa.

Msemaji wa Kremlin Dmitry Peskov, amewaambia waandishi wa habari kwamba kikao hicho cha habari cha kufunga mwaka, hakitafanyika bila kutaja sababu ambazo zimepelekea kikao hicho kutofanyika.

Peskov hata hivyo amesema kwamba Putin amekuwa akizungumza na waandishi wa habari kila mara, ikiwemo anapotembelewa na viongozi kutoka nchi nyingine, na kwamba kiongozi huyo wa Russia atapata fursa nyingine ya kuzungumza na waandishi wa habari.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu