Qatar inasema itaendelea kufanikiwa, kuwepo na kuwa imara licha ya kutengwa kidiplomasia na mataifa sita ya kiarabu kwa madai kuwa inafadhili na kuwaunga mkono magaidi.

In Kimataifa

Qatar inasema itaendelea kufanikiwa, kuwepo na kuwa imara licha ya kutengwa kidiplomasia na mataifa sita ya kiarabu kwa madai kuwa inafadhili na kuwaunga mkono magaidi.

Waziri wa Mambo ya nje wa nchi hiyo Mohammed bin Abdulrahman Al-Thani ameliambia Shirika la Habari la Ufaransa AFP kuwa, Doha inaheshimu sheria na mikataba ya za Kimataifa.

Aidha, amesema kama taifa linaloongoza katika usafirashaji wa gesi nje ya nchi, itaendelea kusafirisha bidhaa hiyo muhimu kwa nchi ya Falme za Kiarabu.

Mataifa yaliyositisha uhusiano wake wa kidiplomasia ni pamoja na Saudi Arabia, Bahrain, Falme za Kiarabu, Yemen, Libya na Misri.

Qatar imekanusha madai dhidi yake na kusema hakuna ushahidi wa kuthibitisha hilo.

Marekani imesema iko tayari kuwaleta pamoja viongozi wa mataifa ya ghuba ili kujadili mzozo huu.

Hata hivyo, Qatar inasema hakuna anayewezesha kushawishi sera yake ya mambo ya nje.

Iran, Kuwait na Uturuki zimependekeza kuwepo kwa mazungumzo ili kumaliza mzozo huu.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu