Qatar inasema itaendelea kufanikiwa, kuwepo na kuwa imara licha ya kutengwa kidiplomasia na mataifa sita ya kiarabu kwa madai kuwa inafadhili na kuwaunga mkono magaidi.

In Kimataifa

Qatar inasema itaendelea kufanikiwa, kuwepo na kuwa imara licha ya kutengwa kidiplomasia na mataifa sita ya kiarabu kwa madai kuwa inafadhili na kuwaunga mkono magaidi.

Waziri wa Mambo ya nje wa nchi hiyo Mohammed bin Abdulrahman Al-Thani ameliambia Shirika la Habari la Ufaransa AFP kuwa, Doha inaheshimu sheria na mikataba ya za Kimataifa.

Aidha, amesema kama taifa linaloongoza katika usafirashaji wa gesi nje ya nchi, itaendelea kusafirisha bidhaa hiyo muhimu kwa nchi ya Falme za Kiarabu.

Mataifa yaliyositisha uhusiano wake wa kidiplomasia ni pamoja na Saudi Arabia, Bahrain, Falme za Kiarabu, Yemen, Libya na Misri.

Qatar imekanusha madai dhidi yake na kusema hakuna ushahidi wa kuthibitisha hilo.

Marekani imesema iko tayari kuwaleta pamoja viongozi wa mataifa ya ghuba ili kujadili mzozo huu.

Hata hivyo, Qatar inasema hakuna anayewezesha kushawishi sera yake ya mambo ya nje.

Iran, Kuwait na Uturuki zimependekeza kuwepo kwa mazungumzo ili kumaliza mzozo huu.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu