Qatar inasema itaendelea kufanikiwa, kuwepo na kuwa imara licha ya kutengwa kidiplomasia na mataifa sita ya kiarabu kwa madai kuwa inafadhili na kuwaunga mkono magaidi.

In Kimataifa

Qatar inasema itaendelea kufanikiwa, kuwepo na kuwa imara licha ya kutengwa kidiplomasia na mataifa sita ya kiarabu kwa madai kuwa inafadhili na kuwaunga mkono magaidi.

Waziri wa Mambo ya nje wa nchi hiyo Mohammed bin Abdulrahman Al-Thani ameliambia Shirika la Habari la Ufaransa AFP kuwa, Doha inaheshimu sheria na mikataba ya za Kimataifa.

Aidha, amesema kama taifa linaloongoza katika usafirashaji wa gesi nje ya nchi, itaendelea kusafirisha bidhaa hiyo muhimu kwa nchi ya Falme za Kiarabu.

Mataifa yaliyositisha uhusiano wake wa kidiplomasia ni pamoja na Saudi Arabia, Bahrain, Falme za Kiarabu, Yemen, Libya na Misri.

Qatar imekanusha madai dhidi yake na kusema hakuna ushahidi wa kuthibitisha hilo.

Marekani imesema iko tayari kuwaleta pamoja viongozi wa mataifa ya ghuba ili kujadili mzozo huu.

Hata hivyo, Qatar inasema hakuna anayewezesha kushawishi sera yake ya mambo ya nje.

Iran, Kuwait na Uturuki zimependekeza kuwepo kwa mazungumzo ili kumaliza mzozo huu.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu