Rafa Benitez akataa kurithi mikoba Goodison Park.

In Kimataifa, Michezo

Rafa Benitez amekataa ofa ya kujiunga na klabu ya Everton, ambayo inatajwa kuwa mbioni kumtimua kazi meneja wao wa sasa Ronald Koeman, kufuatia matokeo mabaya yanayoendelea kuwaandama.

Benitez alikua wa kwanza kwenye orodha ya mameneja wanaopigiwa chepuo kuchukua nafasi ya ukuu wa benchi la ufundi huko Goodison Park, kutokana na kuwa na uzoefu wa kutosha katika ligi ya England.

Benitez mwenye umri wa miaka 57 ametangaza msimamo huo, kwa kuamini bado ana nafasi ya kuendelea kudhihirisha ubora wake akiwa na kikosi cha Newcastle Utd, ambacho alikirejesha ligi kuu msimu uliopita kikitokea ligi daraja la kwanza.

Benitez anaendelea kukumbuka ka kazi nzuri aliyoifanya akiwa na liverpool mwaka 2005, na kufikia mafanikio ya kutwaa ubingwa wa barani Ulaya kwa kuifunga AC Milan.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu