Rais amjulia hali Meja Mstaafu aliyejeruhiwa kwa risasi.

In Kitaifa

Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Dr John Pombe Magufuli, leo ametembelea hospitali ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania JWTZ Lugalo Jijini Dar es Salaam, na kumjulia hali Meja Jenerali Mstaafu Vincent Mribata aliyelazwa hospitalini hapo.

Meja Jenerali Mstaafu Vincent Mribata alishambuliwa na watu wenye silaha, wakati akiingia nyumbani kwake eneo la Ununio, Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu Gerson Msigwa, imeeleza kuwa Mritaba alishambuliwa kwa risasi jana mchana na kisha kupelekwa katika hospitali ya jeshi Lugalo kwa matibabu.

Mkuu wa kituo cha tiba cha hospitali hiyo na daktari bingwa wa magonjwa ya moyo Brigedia Jenerali Paul Massawe, amemueleza Rais Magufuli kuwa Mritaba anaendelea vizuri baada ya madaktari kufanikiwa kutoa risasi alizopigwa mkononi, kiunoni na tumboni.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu