Rais amjulia hali Meja Mstaafu aliyejeruhiwa kwa risasi.

In Kitaifa

Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Dr John Pombe Magufuli, leo ametembelea hospitali ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania JWTZ Lugalo Jijini Dar es Salaam, na kumjulia hali Meja Jenerali Mstaafu Vincent Mribata aliyelazwa hospitalini hapo.

Meja Jenerali Mstaafu Vincent Mribata alishambuliwa na watu wenye silaha, wakati akiingia nyumbani kwake eneo la Ununio, Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu Gerson Msigwa, imeeleza kuwa Mritaba alishambuliwa kwa risasi jana mchana na kisha kupelekwa katika hospitali ya jeshi Lugalo kwa matibabu.

Mkuu wa kituo cha tiba cha hospitali hiyo na daktari bingwa wa magonjwa ya moyo Brigedia Jenerali Paul Massawe, amemueleza Rais Magufuli kuwa Mritaba anaendelea vizuri baada ya madaktari kufanikiwa kutoa risasi alizopigwa mkononi, kiunoni na tumboni.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu