Rais John Magufuli leo anatarajiwa kupokea ripoti ya Kamati ya Pili ya wachumi na wanasheria, iliyochunguza madini yaliyopo kwenye makontena yenye mchanga wa madini.

In Kitaifa

Rais John Magufuli leo anatarajiwa kupokea ripoti ya Kamati ya Pili ya wachumi na wanasheria, iliyochunguza madini yaliyopo kwenye makontena yenye mchanga wa madini.

Anapokea ripoti hiyo ikiwa ni takribani siku 19 tangu alipokabidhiwa ripoti ya mchanga wa madini, iliyoibua madudu na hata kumlazimu kutengua uteuzi wa Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, Kwa mujibu wa taarifa ya Mkurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Gerson Msigwa kwa vyombo vya habari, Rais Magufuli atakabidhiwa ripoti hiyo leo asubuhi Ikulu, Dar es Salaam.

Kamati hiyo ilichunguza aina na viwango vya madini, yaliyomo kwenye mchanga wa madini uliomo ndani ya makontena, yaliyokuwa yamezuiliwa bandarini na Serikali yasisafirishwe kwenda nje ya nchi.

Baada ya kupokea, ripoti hiyo ilionesha mchanga uliokuwa unachunguzwa, ulikuwa na wastani wa kiasi cha thamani kati ya Sh bilioni 829.4 kwa kutumia viwango vya wastani wa chini na Sh trilioni 1.439 kwa kutumia viwango vya juu.

Kutokana na taarifa hiyo, Rais Magufuli aliivunja Bodi ya Wakala wa Ukaguzi wa Madini Tanzania (TMAA), na kumsimamisha kazi Mtendaji Mkuu wa Wakala hiyo kutokana na kutosimamia ipasavyo, mchakato mzima wa usafirishaji mchanga wenye madini nje ya nchi na hivyo kuisababishia nchi hasara kubwa.

Aidha, mbali na kutengua uteuzi wa Waziri Muhongo, alivunja Bodi ya TMAA na kumsimamisha kazi Mtendaji Mkuu wake. Rais Magufuli pia aliviagiza vyombo vya dola, kuwachunguza na kuwachukulia hatua watendaji wa Wizara ya Nishati na Madini na wengine waliohusika na kushindwa kusimamia vema mchakato mzima wa usafirishaji wa mchanga wenye madini nje ya nchi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu