Rais Magufuli amepiga marufuku mpango unaopigiwa kelele kuhusu mwanafunzi anayejifungua kurudi shule.

In Kitaifa

RAIS John Magufuli  amepiga marufuku mpango unaopigiwa kelele  na asasi ziziso za kiserikali, wa kutaka mwanafunzi anayejifungua kurudi shule, kwa maelezo kuwa mpango huo ni laana.

Amesisitiza kuwa kamwe katika kipindi cha uongozi wake, hataruhusu jambo hilo.

Akizungumza  wakati wa kufungua barabara ya Bagamoyo – Msata, Rais Magufuli amesema serikali yake haiko tayari, kutoa Sh bilioni 18.77 kila mwezi kwa ajili ya kusomesha wazazi.

Badala yake, amesema serikali inatoa fedha hizo kwa ajili ya wanafunzi wa shule za msingi hadi sekondari wasome bure.

Ameagiza vyombo vya dola kwamba wakati msichana atabaki nyumbani kulea mtoto, wale wanaohusika kuwapa mimba wanafunzi hao, wakafungwe miaka 30 ili nguvu alizotumia kumpa ujazito, akazitumie kuzalisha mali akiwa gerezani.

 

Katika suala hilo, Rais alisisitiza kuwa hata kama ni mtoto wake akipata ujauzito akiwa shule, kamwe hawezi kurudi shule.

Amezitahadharisha NGO kuwa makini na kunakili mambo ya kigeni kwamba watanakili na mambo ya ajabu, yakiwemo ya ushoga, licha ya kuwa wafadhili wa mambo hayo wanakuja na misaada.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu