Rais Magufuli amepiga marufuku mpango unaopigiwa kelele kuhusu mwanafunzi anayejifungua kurudi shule.

In Kitaifa

RAIS John Magufuli  amepiga marufuku mpango unaopigiwa kelele  na asasi ziziso za kiserikali, wa kutaka mwanafunzi anayejifungua kurudi shule, kwa maelezo kuwa mpango huo ni laana.

Amesisitiza kuwa kamwe katika kipindi cha uongozi wake, hataruhusu jambo hilo.

Akizungumza  wakati wa kufungua barabara ya Bagamoyo – Msata, Rais Magufuli amesema serikali yake haiko tayari, kutoa Sh bilioni 18.77 kila mwezi kwa ajili ya kusomesha wazazi.

Badala yake, amesema serikali inatoa fedha hizo kwa ajili ya wanafunzi wa shule za msingi hadi sekondari wasome bure.

Ameagiza vyombo vya dola kwamba wakati msichana atabaki nyumbani kulea mtoto, wale wanaohusika kuwapa mimba wanafunzi hao, wakafungwe miaka 30 ili nguvu alizotumia kumpa ujazito, akazitumie kuzalisha mali akiwa gerezani.

 

Katika suala hilo, Rais alisisitiza kuwa hata kama ni mtoto wake akipata ujauzito akiwa shule, kamwe hawezi kurudi shule.

Amezitahadharisha NGO kuwa makini na kunakili mambo ya kigeni kwamba watanakili na mambo ya ajabu, yakiwemo ya ushoga, licha ya kuwa wafadhili wa mambo hayo wanakuja na misaada.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu