Rais Magufuli amuagiza Mkurugenzi wa Manispaa ya Moshi kutoa kibali cha ujenzi wa kituo cha Uchunguzi wa Maradhi.

In Kitaifa

Rais John Magufuli amemuagiza Mkurugenzi wa Manisapaa ya Moshi kutoa kibali cha Ujenzi wa Kituo cha Uchunguzi wa maradhi , kilichoombwa na mwananchi mmoja mkoani humo  ili aweze kuendelea na ujenzi huo, kutokana na kutopewa kibali hicho kwa muda mrefu.

Katika hatua nyingine, Rais Magufuli amesema kutokana na Serikali kuzuia unywaji wa pombe aina ya viroba ,idadi ya vifo katika mkoa wa Pwani imepungua kutoka 80 hadi 20, na hata ajali za pikipiki maarufu Bodaboda nazo zimepungua nchini.

Aidha, Rais Magufuli ametaka uongozi wa Wilaya ya Hai kufanya kazi bila kutishwa na madiwani, ikiwa ni pamoja na kubadili sheria ndogondogo wilayani humo ili kupunguza kero za utitiri wa ushuru, kwa wananchi.

Rais Magufuli ametoa maagizo hayo wakati alipokutana na viongozi wa dini wa mkoa wa Kilimanjaro, Vyama vya Siasa na watendaji wa Serikali mkoani humo, na kula nao chakula cha mchana kilichoandaliwa na mkoa wa Kilimanjaro

Raisi  Magufuli yupo Mkoani Kilimanjaro katika ziara yake ya kikazi na natarajiwa kuwa mgeni rasmi katika maaadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani ambayo kitaifa yanaadhimishwa Mkoani Kilimanjaro.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Maagizo ya wizara kuhusu mfuko wa maendeleo ya kilimo.

Naibu Waziri Wa Kilimo Anthony Mavunde, amesema serikaliimeanza kutekeleza uanzishwaji wa mfuko wa maendeleo yakilimo utakaosaidia kukabiliana na changamoto

Read More...

TANZIA: WAZIRI MSTAAFU WA KILIMO AFARIKI DUNIA

Aliyewahi kuwa mbunge wa jimbo la Musoma Vijijini na Waziri wa Kilimo na Mifugo Mhe. Herman Kirigini Amefariki Dunia. Akithibitisha

Read More...

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Professor Makame Mbarawaameliomba Bunge kumuidhinishia kiasi cha Sh Trilioni 3.6ikiwa ni makadirio ya mapato

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu