Rais Magufuli awaagiza watendaji wa serikali kutowabugudhi wamachinga.

In Kitaifa

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Dk.John Pombe Magufuli amewasili jijini Mwanza jana jioni, na kuwaagiza watendaji wa serikali mkoani humo kuacha kuwabugudhi wafanyabiashara ndogondogo maarufu kama wamachinga katika maeneo yao kwani hata wafanyabiashara wakubwa walianza na mitaji midogo kama yao.

Rais magufuli ametoa agizo hilo akiwa njiani kuelekea Ikulu ndogo eneo la Capripoint muda mfupi baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Mwanza, ambapo leo anatarajia kuzindua mradi mkubwa wa maji katika mji wa Sengerema uliogharimu zaidi ya shilingi Bilioni 20 zilizotolewa na Benki ya Maendeleo ya Afrika pamoja na serikali ya Tanzania.

Kauli ya Rais Magufuli inakuja,wakati kukiwa na malalamiko kutoka kwa baadhi ya wamachinga jijini Mwanza wanaodai kusumbuliwa na viongozi pamoja na watendaji wa halmashauri ya jiji la Mwanza,kufuatia kuwepo kwa mgogoro unaoendelea kufukuta uliosababisha wamachinga saba,wakiwemo baadhi ya viongozi wa muungano wa wamachinga mkoani humo kukamatwa na polisi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Serikali kuunga mkono juhudi za Taasisi mbali mbali.

Rais wa Zanzibar Dkt Hussein Mwinyi, amesema serikaliitaendelea kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Taasisi yaZanzibar Maisha Bora Foundation,pamoja na

Read More...

DKT. KIRUSWA AZINDUA MFUMO WA USHIRIKISHWAJI WA WATANZANIA KATIKA SEKTA YA MADINI

Watanzania waendelea kunufaika Sekta ya Madini, ajira 15,341 zamwagwa, manunuzi ya ndani ya nchi yafikia Dola za Marekani bilioni

Read More...

MAFURIKO YAUWA 190 MALAWI

Takriban watu 190 sasa wamethibitishwa kufariki nchini Malawi baada ya Dhoruba ya Mafuriko ya Tropiki Freddy kulikumba eneo

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu