Rais Magufuli awaagiza watendaji wa serikali kutowabugudhi wamachinga.

In Kitaifa

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Dk.John Pombe Magufuli amewasili jijini Mwanza jana jioni, na kuwaagiza watendaji wa serikali mkoani humo kuacha kuwabugudhi wafanyabiashara ndogondogo maarufu kama wamachinga katika maeneo yao kwani hata wafanyabiashara wakubwa walianza na mitaji midogo kama yao.

Rais magufuli ametoa agizo hilo akiwa njiani kuelekea Ikulu ndogo eneo la Capripoint muda mfupi baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Mwanza, ambapo leo anatarajia kuzindua mradi mkubwa wa maji katika mji wa Sengerema uliogharimu zaidi ya shilingi Bilioni 20 zilizotolewa na Benki ya Maendeleo ya Afrika pamoja na serikali ya Tanzania.

Kauli ya Rais Magufuli inakuja,wakati kukiwa na malalamiko kutoka kwa baadhi ya wamachinga jijini Mwanza wanaodai kusumbuliwa na viongozi pamoja na watendaji wa halmashauri ya jiji la Mwanza,kufuatia kuwepo kwa mgogoro unaoendelea kufukuta uliosababisha wamachinga saba,wakiwemo baadhi ya viongozi wa muungano wa wamachinga mkoani humo kukamatwa na polisi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu