Rais Mgufuli aagiza Watumishi 9,932 waliogushi vyeti waondolewe mara moja sambamba na kukatwa mishahara yao.

RAIS wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.JOHN MAGUFULI, amepokea taarifa ya zoezi la uhakiki wa vyeti kwa watumishi wa umma  inayoonyesha uwepo wa watumishi waliogushi vyeti 9,932 na hivyo kuagiza kuondolewa kwenye ajira zao Mara moja.

RAIS MAGUFULI amefikia maamuzi hayo mara baada ya kupokea taarifa hiyo katika ukumbi wa chimwaga uliopo ndani ya chuo kikuu cha DODOMA {udom}, ambapo pia ameagiza kusitishwa kwa mishahara yao ya mwezi huu, pamoja na kuondolewa kwenye orodha ya majina iliyopo hazina na kusisitiza kuwa atakaye kaidi kuondoka hadi tarehe 15 mwezi may mwaka huu, afikishwe kwenye vyombo vya sheria.

Awali  akiwasilisha taarifa hiyo waziri wa nchi ofisi ya rais,utumishi na utawala bora ANGELAH KAIRUKI, amesema kuwa zoezi hilo liliwahusisha watumishi wa umma pekee wakiwemo makatibu wakuu,watendaji na maofisa wa ngazi mbalimbali za serikali, na kuwa zoezi hilo halikuwahusisha viongozi wa kisiasa katika utumishi wa umma wakiwemo wabunge,mawaziri,wakuu wa mikoa na wilaya pamoja na madiwani kwani uteuzi wa nafasi zao ,hufanyika kwa kuwa na sifa ya kujua kusoma na kuandika pekee.

Kwa upande wake waziri wa elimu,sayansi na teknolojia na ufundi JOYCE NDALICHAKO, amewataka wanafunzi kusoma kwa bidii na kuachana na njia za mkato kwani tayari serikali imeziba njia hizo ,hivyo kuwasihi  wanafunzi wote katika taasisi za  elimu ya juu waliojiunga kwa kugushi vyeti kujisalimisha mapema.

Mbali na zoezi la mh.rais kupokea taarifa hiyo ya uhakiki wa vyeti kwa wa watumishi wa umma , pia amezindua maadhimisho ya miaka 10 ya kuanzishwa kwa CHUO KIKUU CHA DODOMA {UDOM}

Exit mobile version