Rais Mugabe achangia dola milioni 1 kwa kuuza ng’ombe.

In Kimataifa

Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe amechangia Umoja wa Afrika (AU) dola za kimarekani milioni 1, baada ya kuuza mamia ya ng’ombe nchini kwake.

Kiongozi huyo amesema kuwa alitoa ng’ombe 300 lakini Wakulima wa Zimbabwe walimuunga mkono na kutoa mara mbili ya idadi hiyo, lengo likiwa kuisadia AU kuondokana na utegemezi wa nchi za Magharibi.

Mugabe alikabidhi hundi ya $1m kwa AU katika mkutano wa viongozi wa Umoja huo uliofanyika nchini Ethiopia, mwanzoni mwa wiki hii.

Mugabe mwenye umri wa miaka 93, wakati akiikabidhi hundi.

Amesema  Kama mkulina na Muafrika, kuchangia ng’ombe ni ishara ya mali, huja kiasilia tu na  suala la AU kujiwezesha kufanikisha shughuli zake yenyewe imekuwa agenda muhimu zaidi katika vikao vya hivi karibuni vya Umoja huo.

Agenda hiyo ilianzishwa kwa nguvu katika mkutano wa 27 wa wakuu wa nchi wanachama uliofanyika jijini Kigali nchini Rwanda, mwaka mmoja uliopita.

Zimbabwe ambayo ilikuwa ikikabiliwa na tatizo la kiuchumi na upungufu wa chakula, mwaka huu umekuwa wa neema kwake kwani nchi hiyo inatarajia mavuno mazuri kulinganisha na miaka iliyopita.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu