Rais Muhammadu Buhari atarajia kurejea nyumbani muda mfupi ujao

In Kimataifa

Kaimu Rais wa Nigeria amesema kuwa Rais Muhammadu Buhari anatarajiwa kurejea nyumbani katika muda mfupi ujao baada ya kuwa jijini London, Uingereza kwa zaidi ya miezi miwili kwa ajili ya matibabu wakati wasiwasi ukizidi kuhusu afya yake.

Makamu wa Rais Yemi Osinbajo amezungumza na waandishi wa habari jana, siku moja baada ya kukutana na Buhari.

Osinbajo amesema Buhari alikuwa katika hali nzuri na anaendelea kupata nafuu haraka. Alisema walizungumza kwa karibu saa moja.

Osinbajo hakutoa maelezo mengine kuhusu afya ya Buhari aliye na umri wa miaka 74, ambaye aliondoka Nigeria kwenda London mnamo Mei 7.

Buhari pia amemaliza karibu wiki saba mjini London mapema mwaka huu, kutokana na matatizo ya kiafya na kisha baadaye akasema hakuwahi kuwa mgonjwa kiasi hicho maishani mwake.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu