Rais Muhammadu Buhari atarajia kurejea nyumbani muda mfupi ujao

In Kimataifa

Kaimu Rais wa Nigeria amesema kuwa Rais Muhammadu Buhari anatarajiwa kurejea nyumbani katika muda mfupi ujao baada ya kuwa jijini London, Uingereza kwa zaidi ya miezi miwili kwa ajili ya matibabu wakati wasiwasi ukizidi kuhusu afya yake.

Makamu wa Rais Yemi Osinbajo amezungumza na waandishi wa habari jana, siku moja baada ya kukutana na Buhari.

Osinbajo amesema Buhari alikuwa katika hali nzuri na anaendelea kupata nafuu haraka. Alisema walizungumza kwa karibu saa moja.

Osinbajo hakutoa maelezo mengine kuhusu afya ya Buhari aliye na umri wa miaka 74, ambaye aliondoka Nigeria kwenda London mnamo Mei 7.

Buhari pia amemaliza karibu wiki saba mjini London mapema mwaka huu, kutokana na matatizo ya kiafya na kisha baadaye akasema hakuwahi kuwa mgonjwa kiasi hicho maishani mwake.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu