Rais Uhuru Kenyatta kuongeza nafasi milioni 6.5 za ajira.

In Kimataifa
Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya anayegombea kuchaguliwa kuwa rais wa Kenya kwa muhula mwingine, ameahidi kuwa serikali yake itaongeza nafasi milioni 6.5 za ajira hasa kwa vijana, na kupunguza bei za vitu katika kipindi cha miaka mitano ijayo.
Rais Kenyatta aliyekuwa anajibu maswali moja kwa moja kupitia facebook kuhusu mipango ya serikali yake kama akichaguliwa, amesema mpango wake utaleta mabadiliko kwenye mafanikio yaliyopatikana katika miaka minne iliyopita.
Mbali na nafasi za ajira, Rais Kenyatta pia amesema atapambana na ufisadi, na kuhakikisha kuwa mahakama inatekeleza wajibu wake ili wahalifu wachukuliwe hatua.
Rais Kenyatta pia ametaka usalama uimarishwe kabla, wakati na baada ya uchaguzi, na kuwakumbusha wakenya kufuata kanuni ya umoja, demokrasia na kuishi kwa masikilizano wakati wakijiandaa na uchaguzi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu