Rais Uhuru Kenyatta kuongeza nafasi milioni 6.5 za ajira.

In Kimataifa
Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya anayegombea kuchaguliwa kuwa rais wa Kenya kwa muhula mwingine, ameahidi kuwa serikali yake itaongeza nafasi milioni 6.5 za ajira hasa kwa vijana, na kupunguza bei za vitu katika kipindi cha miaka mitano ijayo.
Rais Kenyatta aliyekuwa anajibu maswali moja kwa moja kupitia facebook kuhusu mipango ya serikali yake kama akichaguliwa, amesema mpango wake utaleta mabadiliko kwenye mafanikio yaliyopatikana katika miaka minne iliyopita.
Mbali na nafasi za ajira, Rais Kenyatta pia amesema atapambana na ufisadi, na kuhakikisha kuwa mahakama inatekeleza wajibu wake ili wahalifu wachukuliwe hatua.
Rais Kenyatta pia ametaka usalama uimarishwe kabla, wakati na baada ya uchaguzi, na kuwakumbusha wakenya kufuata kanuni ya umoja, demokrasia na kuishi kwa masikilizano wakati wakijiandaa na uchaguzi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu