Rais Uhuru Kenyatta kuongeza nafasi milioni 6.5 za ajira.

In Kimataifa
Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya anayegombea kuchaguliwa kuwa rais wa Kenya kwa muhula mwingine, ameahidi kuwa serikali yake itaongeza nafasi milioni 6.5 za ajira hasa kwa vijana, na kupunguza bei za vitu katika kipindi cha miaka mitano ijayo.
Rais Kenyatta aliyekuwa anajibu maswali moja kwa moja kupitia facebook kuhusu mipango ya serikali yake kama akichaguliwa, amesema mpango wake utaleta mabadiliko kwenye mafanikio yaliyopatikana katika miaka minne iliyopita.
Mbali na nafasi za ajira, Rais Kenyatta pia amesema atapambana na ufisadi, na kuhakikisha kuwa mahakama inatekeleza wajibu wake ili wahalifu wachukuliwe hatua.
Rais Kenyatta pia ametaka usalama uimarishwe kabla, wakati na baada ya uchaguzi, na kuwakumbusha wakenya kufuata kanuni ya umoja, demokrasia na kuishi kwa masikilizano wakati wakijiandaa na uchaguzi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

NACTIVET YASIMAMISHA MAFUNZO CHUO CHA MBEYA TRAINING..DC MALISA AAGIZA KUFANYIWA UHAKIKI VYUO VYOTE WILAYA YA MBEYA

Wazazi Wanafunzi na wahitimu wa chuo cha Mbeya training wameiomba serikali iwasaidie kurudishiwa stahiki zao mara baada ya kubainika

Read More...

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMANNE NOVEMBA 7, 2023

Manchester United na Newcastle United zote zinamfuatilia mshambuliaji wa Lyon Mfaransa Rayan Cherki, 20, ambaye mkataba wake unamalizika Juni

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu