Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta ameonya mahakama nchini humo akiitaka kutousaidia upinzani na kuhujumu uchaguzi unaokuja.

In Kimataifa

Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta ameonya mahakama nchini humo akiitaka kutousaidia upinzani na kuhujumu uchaguzi unaokuja.

Uchaguzi wa urais utafanyika mwezi ujao ambapo uhuru Kenyatta anataka kuchaguliwa tena.

Siku ya Ijumaa, kufuatia kesi iliyowasilishwa mahakamani na upinzani, mahakama kuu iliamrisha tume ya uchaguzi isichapishe makaratasi ya kupigia kura.

Bwana Kenyatta alisisitiza kuwa uchaguzi huo utafanyika jinsi ulivyopangwa,.

Amesema kuwa mahakama hauwezi kudai kuwa huru na kutumia uhuru huo kuingilia idara zingine za serikali.

Muungano wa upinzani wa Nasa ulidai kuwa rais alikuwa na uhusiano na kampuni ya Dubai la Al Ghurair ambayo ilishinda zabuni ya dola milioni 24 kuchapisha makatasi hayo.

Hata hivyo Jaji mkuu wa Kenya David Maraga, ametoa onyo kwa Rais Uhuru Kenyatta kutohujumu imani ya umma juu ya mfumo wa kisheria.

Nayo tume ya Uchaguzi nchini Kenya IEBC leo inatarajiwa kukutana na wagombea wote wanane wa kiti cha uraisi akiwemo Rais Uhuru Kenyata.

Mawakili wa Tume hiyo pia watafika mbele ya mahakama ya rufaa kupata ufafanuzi zaidi juu ya uamuzi huo

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu