Rais wa Marekani Donald Trump alikuwa na mkutano wa pili na Rais wa Urusi Vladimir Putin

In Kimataifa

Rais wa Marekani Donald Trump alikuwa na mkutano wa pili na Rais wa Urusi Vladimir Putin wakati wa mkutano wa kilele wa viongozi wa kundi la G20 uliofanyika Ujerumani mwezi huu, ambao awali haukuwekwa wazi.

Viongozi hao wawili walikutana rasmi kwa mara ya kwanza kwa mazungumzo ya masaa mawili Julai 7 mbele ya vyombo vya habari vya dunia.

Baadaye Trump alisema Putin alikanusha madai kwamba Urusi iliingilia kati uchaguzi wa rais wa Marekani wa mwaka 2016.

Katika mazungumzo yao ya pili ambayo hayakuwekwa wazi awali, Trump na Putin walizungumza kwa zaidi ya saa moja nzima wakiwa pamoja na mkalimani wa Putin.

Mbali na kuwepo kwa wasiwasi kwamba Urusi ilihusika katika kumuweka madarakani Trump, Ian Bremmer, Rais wa Kundi la kimataifa la ushauri wa kisiasa, Eurasia, ameliambia gazeti la Marekani la The Hill kwamba Trump kushiriki mazungumzo hayo bila ya kuwepo mkalimani wake ni kukiuka itifaki ya usalama wa kitaifa.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu