Rais wa Marekani Donald Trump alikuwa na mkutano wa pili na Rais wa Urusi Vladimir Putin

In Kimataifa

Rais wa Marekani Donald Trump alikuwa na mkutano wa pili na Rais wa Urusi Vladimir Putin wakati wa mkutano wa kilele wa viongozi wa kundi la G20 uliofanyika Ujerumani mwezi huu, ambao awali haukuwekwa wazi.

Viongozi hao wawili walikutana rasmi kwa mara ya kwanza kwa mazungumzo ya masaa mawili Julai 7 mbele ya vyombo vya habari vya dunia.

Baadaye Trump alisema Putin alikanusha madai kwamba Urusi iliingilia kati uchaguzi wa rais wa Marekani wa mwaka 2016.

Katika mazungumzo yao ya pili ambayo hayakuwekwa wazi awali, Trump na Putin walizungumza kwa zaidi ya saa moja nzima wakiwa pamoja na mkalimani wa Putin.

Mbali na kuwepo kwa wasiwasi kwamba Urusi ilihusika katika kumuweka madarakani Trump, Ian Bremmer, Rais wa Kundi la kimataifa la ushauri wa kisiasa, Eurasia, ameliambia gazeti la Marekani la The Hill kwamba Trump kushiriki mazungumzo hayo bila ya kuwepo mkalimani wake ni kukiuka itifaki ya usalama wa kitaifa.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu