Rais wa Marekani Donald Trump amesema kuwa kuna haja ya kukabiliana na itikadi kali katika dini ya kiislamu wakati akitoa hotuba yake nchini Saudi Arabia.

In Kimataifa

Rais wa Marekani Donald Trump amesema kuwa kuna haja ya kukabiliana na itikadi kali katika dini ya kiislamu wakati akitoa hotuba yake nchini Saudi Arabia.

Akiongea kwenye kwenye mji mkuu wa Riyadh, alisema kuwa vita dhidi ya itikadi kali sio vita kati ya imani tofauti bali vita kati ya mambo mazuri na yale maovu.

Trump ambaye yuko kwenye ziara yake ya kwanza katika nchi za kigeni, alizungumza wakati wa mkutano wa viongozi wa kikanda.

Hata hivyo hotuba yake Trump inaonekama kama njia ya kutafuta uungwaji mkono katika vita dhidi ya wanamgambo wa Islamic State.

Hatua yake ya hivi majuzi ya kupiga marufuku safari ya kwenda Marekani kwa raia wa mataifa 7 yenye waislamu wengi duniani, ilisababisha hasira kote katika mataifa ya kiislamu.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Maagizo ya wizara kuhusu mfuko wa maendeleo ya kilimo.

Naibu Waziri Wa Kilimo Anthony Mavunde, amesema serikaliimeanza kutekeleza uanzishwaji wa mfuko wa maendeleo yakilimo utakaosaidia kukabiliana na changamoto

Read More...

TANZIA: WAZIRI MSTAAFU WA KILIMO AFARIKI DUNIA

Aliyewahi kuwa mbunge wa jimbo la Musoma Vijijini na Waziri wa Kilimo na Mifugo Mhe. Herman Kirigini Amefariki Dunia. Akithibitisha

Read More...

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Professor Makame Mbarawaameliomba Bunge kumuidhinishia kiasi cha Sh Trilioni 3.6ikiwa ni makadirio ya mapato

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu