Rais wa Marekani Donald Trump amewaambia washirika wa Marekani katika shirika la kujihami la mataifa ya Magharibi, Nato, mjini Brussels kwamba washirika wote ni lazima wagharimie sehemu yao ya gharama ya matumizi ya kijeshi.

In Kimataifa

Rais wa Marekani Donald Trump amewaambia washirika wa Marekani katika shirika la kujihami la mataifa ya Magharibi, Nato, mjini Brussels kwamba washirika wote ni lazima wagharimie sehemu yao ya gharama ya matumizi ya kijeshi.

Ni “kiasi kikubwa sana cha pesa” ambacho hakijalipwa, alisema, na kukariri wasiwasi ambao umekuwepo kwamba Marekani imekuwa ikilipa fedha zaidi kuliko washirika wake.

Bw Trump pia amelaani shambulio la bomu la Manchester lililotekelezwa Jumatatu na kusema kwamba ugaidi shari ukomeshwe.

Alitoa wito wa kuwepo kwa kipindi cha kimya kwa heshima ya watu 22, watu wazima na watoto, waliouawa katika “shambulio hilo la kikatili”.

Bw Trump pia ameonya kuhusu hatari ambayo inaletwa na kuruhusiwa kwa watu kuhama bila kudhibitiwa na pia hatari inayotokana na urusi.

Kabla ya kuzuru makao makuu ya Nato, Bw Trump alikutana na viongozi kadha wa EU kwa mara ya kwanza, wakiwemo rais mpya wa Ufaransa Emmanuel Macron.

 

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu