Rais wa Marekani Donald Trump amewaambia washirika wa Marekani katika shirika la kujihami la mataifa ya Magharibi, Nato, mjini Brussels kwamba washirika wote ni lazima wagharimie sehemu yao ya gharama ya matumizi ya kijeshi.

In Kimataifa

Rais wa Marekani Donald Trump amewaambia washirika wa Marekani katika shirika la kujihami la mataifa ya Magharibi, Nato, mjini Brussels kwamba washirika wote ni lazima wagharimie sehemu yao ya gharama ya matumizi ya kijeshi.

Ni “kiasi kikubwa sana cha pesa” ambacho hakijalipwa, alisema, na kukariri wasiwasi ambao umekuwepo kwamba Marekani imekuwa ikilipa fedha zaidi kuliko washirika wake.

Bw Trump pia amelaani shambulio la bomu la Manchester lililotekelezwa Jumatatu na kusema kwamba ugaidi shari ukomeshwe.

Alitoa wito wa kuwepo kwa kipindi cha kimya kwa heshima ya watu 22, watu wazima na watoto, waliouawa katika “shambulio hilo la kikatili”.

Bw Trump pia ameonya kuhusu hatari ambayo inaletwa na kuruhusiwa kwa watu kuhama bila kudhibitiwa na pia hatari inayotokana na urusi.

Kabla ya kuzuru makao makuu ya Nato, Bw Trump alikutana na viongozi kadha wa EU kwa mara ya kwanza, wakiwemo rais mpya wa Ufaransa Emmanuel Macron.

 

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu