Rais wa Somalia ameyataka mataifa makubwa duniani kumsaidia kupambana na magaidi.

In Kimataifa

Rais wa Somalia Mohammed Abdullahi Mohammed ameyataka mataifa makubwa duniani kumsaidia kupambana na magaidi , rushwa na umasikini, katika mkutano wa kimataifa wenye lengo la kuimarisha taifa hilo lililoharibiwa kwa mizozo chini ya uongozi mpya.

Mohamed Abdullahi ameuambia mkutano huo mjini Landon kwamba taifa hilo lililoharibiwa kwa mizozo linaweza kuneemeka kutokana na uwezo wa jadi wa Wasomali wa kufanya biashara iwapo linaweza kuzuwia kitisho cha njaa , uharamia na itikadi kali ya kiislamu.

Mkutano huo wa siku moja , uliohudhuriwa na viongozi mbali mbali duniani, unataka kufikiwa makubaliano mapya kati ya Somalia na mtandao wa waungaji wake mkono wa kimataifa kuharakisha maendeleo katika masuala ya usalama, maendeleo na uchumi ifikapo mwaka 2020.

Taifa hilo la Afrika mashariki lenye matatizo , ambalo mara kwa mara limekuwa juu katika faharasa ya mataifa dhaifu , limepata rais , waziri na bunge jipya mwaka huu na mkutano huo unalenga kuweka uthabiti katika kundi hilo la viongozi

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu