Rais wa Somalia ameyataka mataifa makubwa duniani kumsaidia kupambana na magaidi.

In Kimataifa

Rais wa Somalia Mohammed Abdullahi Mohammed ameyataka mataifa makubwa duniani kumsaidia kupambana na magaidi , rushwa na umasikini, katika mkutano wa kimataifa wenye lengo la kuimarisha taifa hilo lililoharibiwa kwa mizozo chini ya uongozi mpya.

Mohamed Abdullahi ameuambia mkutano huo mjini Landon kwamba taifa hilo lililoharibiwa kwa mizozo linaweza kuneemeka kutokana na uwezo wa jadi wa Wasomali wa kufanya biashara iwapo linaweza kuzuwia kitisho cha njaa , uharamia na itikadi kali ya kiislamu.

Mkutano huo wa siku moja , uliohudhuriwa na viongozi mbali mbali duniani, unataka kufikiwa makubaliano mapya kati ya Somalia na mtandao wa waungaji wake mkono wa kimataifa kuharakisha maendeleo katika masuala ya usalama, maendeleo na uchumi ifikapo mwaka 2020.

Taifa hilo la Afrika mashariki lenye matatizo , ambalo mara kwa mara limekuwa juu katika faharasa ya mataifa dhaifu , limepata rais , waziri na bunge jipya mwaka huu na mkutano huo unalenga kuweka uthabiti katika kundi hilo la viongozi

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu