Rais wa Somalia atangaza vita dhidi ya Al Shabab, awataka kujisalimisha.

In Kimataifa

Rais wa Somalia Mohamed Abdullahi “Farmajo” ametangaza vita dhidi ya wanamgambo wa Al Shabab.

Farmajo ambaye amekuwa rais kwa miezi minne, ameongeza kuwa anatoa siku 60 kwa wanamgambo hao kujisalimisha.

Amefafanua kuwa ikiwa watajisalimisha, watapewa mafunzo ya kijeshi, watapewa elimu na kuajiriwa na serikai ya Mogadishu.

Kauli hii ya kiongozi huyu wa Somalia inakuja siku moja baada ya shambulizi la bomu mjini Mogadishu na kusababisha vifo vya watu saba na kuwajeruhi wengine.

Amesisitiza kuwa maafisa wa usalama wamejipanga ipasavyo kuhakikisha kuwa mashambulizi ya Al Shabab hayatokei tena na wanakabiliwa ipasavyo.

Hivi karibuni, rais Farmajo aliwabadilisha maafisa wa usalama katika idara ya ujasusi katika juhudi za kukabiliana na Al Shabab.

Rais huyo ameyasema haya mjini Mogadishu ikiwa amevalia sare za kijeshi pamoja na Waziri wake Mkuu Hassan Ali Khayre, na kutoa wito kwa raia wa nchi hiyo kuunga mkono juhudi za wanajeshi.

Kundi la Al Shabab ambalo lilianza mashambulizi yake nchini Somalia mwaka 2006, limesababisha mamia ya watu kupoteza maisha nchini Somalia na katika nchi jirani kama Kenya na Uganda.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Maagizo ya wizara kuhusu mfuko wa maendeleo ya kilimo.

Naibu Waziri Wa Kilimo Anthony Mavunde, amesema serikaliimeanza kutekeleza uanzishwaji wa mfuko wa maendeleo yakilimo utakaosaidia kukabiliana na changamoto

Read More...

TANZIA: WAZIRI MSTAAFU WA KILIMO AFARIKI DUNIA

Aliyewahi kuwa mbunge wa jimbo la Musoma Vijijini na Waziri wa Kilimo na Mifugo Mhe. Herman Kirigini Amefariki Dunia. Akithibitisha

Read More...

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Professor Makame Mbarawaameliomba Bunge kumuidhinishia kiasi cha Sh Trilioni 3.6ikiwa ni makadirio ya mapato

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu