Rais wa Sudan Kusini ametangaza hali ya hatari kwa muda wa miezi mitatu katika jimbo la Gogrial.

In Kimataifa

Rais Salva Kiir  wa Sudan Kusini ametangaza hali ya hatari kwa muda wa miezi mitatu katika jimbo la Gogrial, ambako mapigano yamekuwa yakiendelea kwa miezi kadhaa, kati ya wanamgambo kutoka koo za Apuk na Aguok za kabila la Dinka, analotokea Kiir.

Msemaji wa serikali amesema hapo jana.

Michael Makuei, ambaye pia ni waziri wa habari, amesema jeshi litapewa mamlaka maalum kuzuia mapigano katika jimbo hilo la Gogrial, na kwamba haki za raia zitasitishwa, licha ya kwamba rais hajatangaza ni haki gani zitaathirika.

Makuei alisema watu wapatao 70 waliuawa katika mapigano ya mwezi Mei.

Makuei amesema hali ya hatari pia inahusu katika maeneo jirani ya Tonj, Wau na Aweil mashariki.

 

 

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu