Rais wa Sudan Kusini ametangaza hali ya hatari kwa muda wa miezi mitatu katika jimbo la Gogrial.

In Kimataifa

Rais Salva Kiir  wa Sudan Kusini ametangaza hali ya hatari kwa muda wa miezi mitatu katika jimbo la Gogrial, ambako mapigano yamekuwa yakiendelea kwa miezi kadhaa, kati ya wanamgambo kutoka koo za Apuk na Aguok za kabila la Dinka, analotokea Kiir.

Msemaji wa serikali amesema hapo jana.

Michael Makuei, ambaye pia ni waziri wa habari, amesema jeshi litapewa mamlaka maalum kuzuia mapigano katika jimbo hilo la Gogrial, na kwamba haki za raia zitasitishwa, licha ya kwamba rais hajatangaza ni haki gani zitaathirika.

Makuei alisema watu wapatao 70 waliuawa katika mapigano ya mwezi Mei.

Makuei amesema hali ya hatari pia inahusu katika maeneo jirani ya Tonj, Wau na Aweil mashariki.

 

 

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu